Thursday 10 July 2014

Hebu jiulize masuala haya.....


HEBU jiulize masuala haya na lifikirie katika akili yako kila suala jibu utapata mwenyewe 
Mimi ni nani katika hii dunia?

Nimeishi miaka mingapi hadi sasa?

Nimebakiza miaka mingapi ya kuishi?

Nimefanya mangapi kwa ajili ya akhera yangu?

Maovu mangapi nimetenda kwa kuteleza au kwa makusudi?

Lini nilitoa chozi kutubu mabaya yangu? 

Lini nilikaa faragha na kumshukuru M/Mungu kwa wema anaonitendea? 

Hivi Mungu akichukua roho yangu wakati huu, nimebeba kazi (amali) ngapi za kheri zitakazo nisaidia?.

Nitakumbukwa kwa wema gani niliowatendea wanadamu na viumbe wengine?

ZINDUKA NDUGU YANGU.DUNIA ISITUHADAE TUKAMSAHAU MUNGU. Wakumbushe na wengine.

1 comment: