Thursday 10 July 2014

Nasaha Muhimu


Anza siku yako kwa kumtaja na kumkumbuka Mungu katika nyakati za asubuhi upate kufaulu.

Endelea na kuomba msamaha kwa Mungu mpaka shetani akaribie kujiua.

Usiache dua kwani ndio kamba ya uokofu.

Kumbuka maneno yako yanaandikwa na malaika.

Kua na matarajio mema hata kama uko katika kidimbwi cha kimbunga (matatizo).

Uzuri wa vidole ni kuvifungamanisha na tasbih.

Wasiwasi na dhiki zikizidi sema: "LAA ILAHA ILLA ALLAH."

Nunua dua ya fakiri na mapenzi ya maskini kwa pesa.

Sijda ndefu kwa ajili ya Mungu yenye unyenyekevu ni bora kuliko makasri mazuri (Majumba ya kifakhari).

Fikiri kabla hujatoa neno kwani huenda neno likaua.

Jihadhari na dua ya madhlum na chozi la mwenye kunyimwa (maskini).

Kabla kusoma vitabu na magazeti: soma 
Qur-an.

Tengeza sababu ya kunyooka watu wako.

Jitahidi nafsi yako katika utiifu kwani nafsi ni yenye kuamrisha maovu sana.

Busu viganja vya wazazi wako utapata radhi.

Nguo zako kuukuu ni mpya kwa mafukara.

Usighadhibike (usikasirike) maisha ni mafupi kuliko unavyodhania.

Uko na mwenye nguvu wa wenye nguvu na tajiri wa matajiri naye ni Mungu Aliyetukuka.

Wingi wa kutoka kwako pasi na haja ni inadi na uovu.

Usifunge mlango wa kabuli kwa maasi.

Sala ni kitu bora cha kukusaidia kwenye misiba na machofu.

Jiepushe na dhana mbaya utapumzisha watu na utapumzika wewe mwenyewe pia.

Sababu ya kila dhiki ni kumpa nyongo Mungu basi mkabili (muendee).

Sali sala utakayoingia nayo kaburini mwako.

Ukimsikia asi anasengenya mwambie: mche Mwenyezi Mungu.

Dumu katika kusoma surat Tabaraka kwani inaokoa.

Mwenye kunyimwa (maskini) ni aliyenyimwa sala ya unyenyekevu na jicho la kutoa machozi.

Usimuudhi muumini.

Fanya mapenzi yako yote kwa Mungu na Mitume wake saw.

Msamehe aliyekusengenya kwani amekupa thawabu zake.

sala, kusoma Qur-an na kumkumbuka Mungu ni mafungamano ya kunawiri kifuani mwako.

Anayekumbuka joto la moto anasubiria sababu za maasi.

Madamu usiku hupita basi uchungu utaondoka, na matatizo yatatatuka na shida itapita.

Epuka kusengenya (qiila wa qaala: alisema, kulisemwa)kwani una amali kama majabali.

Sali kwa unyenyekevu kwani yote yanayokusubiri si muhimu kuliko sala.

Weke Qur-an kichwani kwako kwani kuisoma aya moja ni bora kuliko dunia na vilivyomo ndani yake.

Maisha ni mazuri na kizuri zaidi ni wewe kwa imani yako na tabia yako na heshima yako.

1 comment:

  1. Nasaha yenye kupigiwa mfano katika jamii,hususan kimsingi na kimaisha haswa waliofika tamati na kukata tamaa.

    ReplyDelete