Sunday 31 August 2014

Muenzi Mke Wako

Imeandikwa na Shaykh 'Abdullaah 'Adhamiy

Imefasiriwa na Iliyaasa

Kwa kuoa huchukui tu mke, Bali unachukua ulimwengu wako mzima. Kuanzia hapo mpaka maisha yako yote mke wako atakuwa mwenzio, mwandani wako, na rafiki yako mpenzi.

Atashiriki katika nyakati zako nzuri, siku zako, na miaka yako. Atakuwa pamoja nawe katika furaha na shida, katika mafanikio na tabu, katika ndoto zako na katika wakati wa hofu. Ukiumwa, atakupa huduma bora kabisa. Wakati unapohitaji msaada atafanya vyovyote awezavyo kwa ajili yako. Wakati una siri, ataitunza siri yako, wakati unahitaji ushauri, atakupa ushauri mzuri kabisa.

Atakuwa na wewe utakapoamka asubuhi kitu cha kwanza ambacho macho yako yataona ni macho yake. Wakati wa mchana, atakuwa na wewe, kama kuna wakati mchache hatokuwa na wewe kwa kimwili, atakuwa anakufikiria wewe, anakuombea dua kwa moyo wake wote, akili yake yote, na roho yake nyote. Ukienda kulala usiku, kitu cha mwisho macho yako kuona itakuwa ni yeye, na ukilala bado utakuwa unamuona katika ndoto zako. Kwa kifupi atakuwa ni ulimwengu wako mzima na wewe utakuwa ulimwengu wake mzima.  

Kielezo bora kabisa ambacho mimi binafsi nishawahi kusoma kinafafanua ukaribu wawanandoa juu ya wao kwa wao na kielezo hicho kipo katika aya ya Qur-aan ambayo inasema:

((Wao ni vazi kwenu, na nyinyi ni vazi kwao)) [Al-Baqarah 2:187].

Na Kweli, wanandoa ni kama vazi juu ya wao kwa wao kwa sababu wanapeana ulinzi, liwazo, kinga (stara), msaada (tegemeo), na mapambo ambayo vazi linampa mtu. Hebu jaribu kufikiri msafara wakati wa siku za baridi kwenda sehemu kama vile Alaska bila ya kuwa na nguo! Wanandoa wetu wanatupa kiwango kile kile cha faraja (liwazo), ulinzi, na msaada  katika msafara wa maisha yetu katika dunia hii kama vile nguo itakavyofanya katika msafara wa Alaska.

Mahusiano baina ya wanandoa ni ya kustaajabisha kabisa katika mahusiano yote ya kibinaadamu: Idadi ya mapenzi na mahaba, undani na ukaribu, huruma na imani, amani na utulivu ambao unajaza nyoyo za wanandoa ni jambo lisiloelezeka kwa wepesi. Ufafanuzi pekee wa mantiki ambao unaweza kuelezeka juu ya haya mastaajabu makubwa katika hisia zote za kibinaadamu ni kwamba: Ni kitendo cha Allah Subhanahu wa Ta'ala, ((Na Allaah Amekuumbieni wake [na wenza katika jinsi yenu])) [An-Nahl 16:72]

Mola wetu tu Allaah Subhanahu wa Ta'ala katika katika Utawala Wake usio na upeo wa huruma Yake  isiyo na mipaka  na Hekima Yake adhimu Anaweza kujenga na kuzididimiza katika akili hizi hisia za kustaajabisha na za kubarikiwa katika nyoyo za wanandoa. Kwa kweli Allah Subhanahu wa Ta'aala Anawakumbusha wale ambao wanatafuta ishara Zake katika ulimwengu huu kwamba hisia hizi katika moyo wa wanandoa ni katika ishara Zake ambazo zinatakiwa zimuongoze mwanaadamu katika kuwepo Kwake kama Alivyosema katika Qur-aan, (Na katika Ishara Zake ni kuwa Amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye Amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo ishara kwa watu wanaofikiri." [Ar-Ruum 30:21]

Lakini Allaah Subhanahu Wa Ta’aala Anajua kwamba moyo wa binaadamu sio kitu ambacho kiko tuli, wakati mwengine huwa dhaifu na wakati mwengine huwa na nguvu. Hisia zinaweza kubadilika na hubadilika pindi wakati unavyosogea. Mapenzi yanaweza kufifia na kupayuka mbalini. Mshikamano wa ndoa unaweza kuwa dhaifu kama haujahudumiwa vizuri. Furaha katika ndoa haiwezi kudharauliwa; furaha ya kuendelea inahitaji utowaji wa daima kutoka pande zote. Ili mti wa mapenzi ya ndoa ubaki hai na kuendelea kuishi, udongo lazima udumishwe, uhifadhiwe, umwagiwe maji na ulelewe.

Kumbuka kwamba Mtume wetu Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipata nafasi ya kwenda kwenye majangwa na kushindana mbio na mke wake Bibi 'Aaishah. Bibi 'Aaishah alimshinda Mtume lakini baadae aliponenepa, Mtume alimshinda Bibi 'Aaishah. Kumbuka kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimchukua mkewe kwenda kuwatazama vijana wa Ki-Ethiopia wakicheza michezo ya utamaduni wao. Maonyesho ya hisia yanahitajika kuweza kuufanya mshikamano wa ndoa usifanye kutu na kuoza. Kumbuka kwamba utapata thawabu kutoka kwa Allah (Subhanahu wa Ta'aala) kwa hisia zozote unazomuonyesha mkeo kamaMtume   (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alivyosema: ((Mmoja wenu atapata thawabu kwa chochote ambacho atafanya ili kutafuta radhi za Allaah hata kwa tonge analomlisha mkewe))

Kamwe usidharau umuhimu wa vitu vidogo vidogo kama vile kuweka chakula kwenye mdomo wa mkeo, kumfungulia mlango wa gari, na hali kadhalika. Kumbuka kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anasogeza goti lake kwa mkewe amkanyage kuweza kumpanda ngamia.

Jaribu kutafuta wakati ili nyote wawili muweze kuswali pamoja. Kuuimarisha uhusiano kati yenu na Allaah (Subhanahu wa Ta'aala) ni hakikisho kubwa kuwa uhusiano wenu wa kindoa utabaki madhubuti. Kuwa na amani kati yenu na Allah (Subhanahu wa Ta'ala)  daima kutapelekea ndani mwenu kuwa na amani zaidi.

Kumbuka kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliwapa habari nzuri (aliwabashiria) wanandoa wanaoamka usiku kuswali pamoja. Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anamsisitiza mwanandoa anayeamka mwanzo amuamshe mwenzake, japo kummwagia maji katika uso wake. 

Daima jaribu uwezavyo kuwa mtu mzuri kwa mkeo kwa njia ya maneno na vitendo. Ongea nae, mchekee, tafuta ushauri wake, muulize juu ya mawazo yake, tumia wakati maalum na yeye na daima kumbuka kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema:((Wabora katika nyinyi ni wale ambao ni wabora kwa wake zao))

Mwishowe, ni kawaida kwa wanandoa kuahidi kuwapenda na kuwaheshimu wanandoa wenziwe mpaka mauti yawatenganishe. Naamini kwamba ahadi hii ni nzuri au ni bora kabisa, lakini haitoshi! Haitoshi kumpenda mkeo tu. Lazima upende anachokipenda pia. amilia yake, anaowapenda yeye uwapende pia. Usiwe kama mwenzangu mmoja ambaye hakufurahiwa kuja kwa wazazi wa mke wake kukaa kwa wiki chache. Alimwambia wazi mkewe “Mimi siwapendi wazazi wako”. Bila ya kusita mkewealimtazama machoni kwa hasira na kusema, “Na wako pia siwapendi”.

Mapenzi yasiishe na pia tunaamini kuna maisha baada ya mauti ambapo wale ambao walifanya wema katika dunia hii wataungana na wanandoa wenzio ((Ingieni Peponi, nyinyi na wake zenu; mtafurahishwa humo)) [Az-Zukhruf 43:70] Pia wataungana na watoto wao.

Na mfano bora katika mintarafu hii itakuwa ni Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ambaye mapenzi yake kwa Bibi Khadiyjah, mkewe aliyeishi naye kwa miaka 25 yalisogea mpaka kwa wale aliowapenda Khadiyjah; mapenzi yake haya yaliendelea hata baada ya kufa Bibi Khadiyjah. Ilikuwa miaka mingi baada ya kifo cha Bibi Khadiyjah na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakumsahau na kila panapochinjwa mbuzi katika nyumba yake basi hutuma kifurushi kwa familia ya Bibi Khadiyjah na marafiki zake na kila akihisi kuwa mgeni  anayegonga mlango ni Dada ya Khadiyjah aitwaye Hala, Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiomba huku akisema, "Ee Allaah Jaalia awe ni  Hala."

Tuesday 19 August 2014

Zingatia haya yatakusaidia

Kuachana na swala inamaanisha kwamba utakosa raha ya nafsi katika dunia hii..amesema Mwenyezi Mungu: Na anayepingana na utajo wangu hakika atapata maisha ya dhiki

Hao ni wenye matumaini wale wanaoshibisha roho yako tamaa na kukusukuma kufanya kazi, wanakuliwaza kwa hekima kutokana na mateso yako na wanayapoza, na wanairutubisha furaha yako na wanatia nguvu ndoto yako na wanaiamsha..hao wafanye marafiki

Kama unataka kugeuza nafsi yako na kuipaisha kwa kiwango bora, huna budi utambue kwamba hatua ya kwanza ya mageuzi inatoka ndani yako... mageuzi yanaanza kwa nia ya mageuzi

Juu yenu kutubu.. kwani ina faida kwenu kuliko faida ya upanga
-alfudhail bin 'ayyaadh

Kuwa mtu mwema kwa unaowapita wakati unapanda kileleni.. kwani utakutana nao wakati unateremka! hakuna mmoja anayebaki kileleni maisha yote
  -steven cofey

Mtume Muhammad SAW alikusanya baina ya taqwa na tabia njema, kwani kumcha Mwenyezi Mungu ni baina ya mja na Mola wake, na tabia njema ni baina yake na viumbe
   -ibn alqayyim

(watapambwa kwa bangili za dhahabu) peponi; mapambo kwa wote, wanaume na wanawake..ni peponi.. huko kuna vinavyotamanisha nafsi na kuburudisha macho na kayafurahisha

Imepokewa na Jarir bin Abdallah amesema: Amesema Mtume SAW:

Amesema Mtume Muhammad SAW: hakika salaam (amani) ni jina miongoni mwa majina ya Allah SW lililowekwa kwenye ardhi, basi enezeni salamu baina yenu>>

Amiliana kwa wema kwa anayestahiki na asiyestahiki, kwani wewe unatafuta nyumba ya peponi si nyumba kwenye moyo wa kila mtu

Izoeshe nafsi yako kwenye mambo matatu:
- ukifanya jambo kumbuka Mola anakuona,
-na ukiongea ujue Mola amekusikia,
-na ukinyamaza elewa kwamba Mola anajua unachofikiri
  -hatim al asam

Wanadamu ni watu wa ajabu.. wanatenda kwa ajili ya dunia, huku wakiruzukiwa bila  amali..na wala hawafanyi kwa ajili ya akhera, ambapo hawataruzukiwa ila kwa amali

Kuchora tabasamu ni jambo jepesi ambalo unalifanya na kwa ujira mkubwa

Kila kitu inawezekana kukinunua ila nia nzuri, hiyo chimbuko lake linatoka kwenye kisima cha kichawi ndani ya nyoyo safi

Kila starehe isiyokuwa kwa ajili ya Allah, itabadilika na kuwa majuto kwa aliyeifanya siku ambayo ukubwa wake ni miaka elfu hamsini! mwenye akili ni yule anayestarehe mara mbili.. hapa duniani kwa twaa ya Mwenyezi Mungu, kisha peponi

Jiondoshee hisia za mateso, na mateso yenyewe yataondoka
-marcus aurelios

Mvivu hahisi thamani ya raha, kinyume na mchapa kazi ambaye anifurahia baada kufanya juhudi, akitaka kurudisha nguvu zake

Ewe Mola waponye wagonjwa waislamu, na walishe wenye njaa, na warudishe waliopotea, na waachie huru wafungwa wao, na warehemu maiti wao, na wape usalama na amani popote walipo katika ardhi hii ewe Mola wa viumbe vyote

       