Thursday 10 July 2014

Hebu jiulize masuala haya.....


HEBU jiulize masuala haya na lifikirie katika akili yako kila suala jibu utapata mwenyewe 
Mimi ni nani katika hii dunia?

Nimeishi miaka mingapi hadi sasa?

Nimebakiza miaka mingapi ya kuishi?

Nimefanya mangapi kwa ajili ya akhera yangu?

Maovu mangapi nimetenda kwa kuteleza au kwa makusudi?

Lini nilitoa chozi kutubu mabaya yangu? 

Lini nilikaa faragha na kumshukuru M/Mungu kwa wema anaonitendea? 

Hivi Mungu akichukua roho yangu wakati huu, nimebeba kazi (amali) ngapi za kheri zitakazo nisaidia?.

Nitakumbukwa kwa wema gani niliowatendea wanadamu na viumbe wengine?

ZINDUKA NDUGU YANGU.DUNIA ISITUHADAE TUKAMSAHAU MUNGU. Wakumbushe na wengine.

Hakika Halali Iko Wazi Na Haramu Iko Wazi


Kutoka kwa- Abu Abdullah An-Nu’uman Ibn Bashiyr -(RA) -ambaye alisema: Nilimsikia Mtume Mohammad (SAW) akisema:

Halali iko wazi na haramu iko wazi, baina yao ni vitu vyenye shaka ambavyo watu wengi hawajui.-- Kwa hivyo, yule anayeepuka vyenye shaka- anajisafisha nafsi yake kwenye dini yake na heshima yake, lakini yule anayetumbukia katika mambo yenye shaka, huanguka katika haramu, kama mchungaji anayechunga (wanyama) pembezoni mwa mpaka, mara- huingia ndani (ya shamba la mtu).- Hakika kila mfalme ana mipaka yake, na mipaka ya Mwenyezi Mungu ni makatazo Yake. Na hakika katika kiwiliwili kuna kipande cha nyama kikitangamaa, kiwiliwili chote hutangamaa, na kikharibika kiwiliwili chote huharibika. Basi jua (kipande hicho cha nyama) ni moyo.

Imesimuliwa na Al-Bukhari na Muslim

Wasia wa Luqman Kwa Mwanae (Na kwetu sisi sote)


Assalam Alaykum Warahmatullah Wabarakatuh;

Katika makala hii fupi, utapata ingawa kwa ufupi wasia alioutowa luqman kwa mwanae. Kwa hikma ya kisa hiki cha mja huyu mwema ndani ya Qur’an ni kwa malengo yetu sote na pili umuhimu wetu kuwa nasihi watoto wetu katika ibada.

Katika nasaha alizompatia mwanawe ni kuwatendea wema wazazi, kutokua na kibri, kusimamisha Swalah, kuamrisha mema na kukataza maovu, kusubiri, kutonyanyua sauti na kadhalika kama Alivyotupa maelezo hayo Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):

‘Ewe mwanangu! Kikiwapo kitu cha uzito wa chembe ya khardali kikawa ndani ya jabali au ndani ya mbingu au ndani ya ardhi, basi Allaah Atakileta. Hakika Allaah ni Mjuzi wa yaliyofichika, Mwenye khabari za yote’. -

‘Ewe mwanangu! Shika Swalah, na amrisha mema, na kataza maovu, na subiri kwa yanayo kupata. Hayo ni katika mambo ya kuazimiwa’

‘Wala usiwabeuwe watu, wala usitembee katika nchi kwa maringo. Hakika Allaah Hampendi kila anayejivuna na kujifakhirisha‘ [Luqmaan:16-18]
Mahmoud Al-Asmi at 18:30

Kuwadanganya wanawake


Mmoja wa wenye hikma alisema: 
Jihadhari na kuwadanganya wanawake, kwani wana uhodari wa kujua ukweli, na uwezo mkubwa wa kujifanya hawajajua...!

"Mwenye kupoteza penzi la mwanamke muaminifu, amepoteza maisha yake yote"

- Je unajua kwamba......

1- mwanamke akiwasiliana nawe sana inamaanisha hataki kuongea na mwengine..?

2- mwanamke atapata mwanamme bora kuliko wewe kwasababu amejifunza kuchagua kwa jeraha lake.....

3- mwanamke aliyedhulumiwa, mwanamme atamrudia wakati akiwa ameshachelewa... (too late..!!)

4- mwanamke anamiliki hisia ya sita zaidi ya mwanamme kumjua akibadilika au akimkhuni.......!

5- mwanamke anasubiri na kuvumilia sana kuliko mwanamume.. na akimuacha mwanamme basi ni baada ya kujaribu kumuomba msamaha mara elfu..

6- mara nyingi mwanamke akiungulika anapendelea kunyamaza.....

7- mwanamke anaporeact na kukulaumu hii inamaanisha mapenzi yake mingi kwako...

8- mwanamke anapokua amekerwa na mwanamme ananyamaza kwa kutaraji kuwa atabadilika na sio kwa kutojua....

9- mwanamke akizungumziwa na mwanamme kuhusu mwanamke mwengine, huficha kilio chake nyuma ya tabasamu lake......

Mtume Mohammed (saw) kamfananisha mwanamke na chupa ya kiyoo tuibebe pole pole isituponyoke ikavunjika

Na maana yake tuishi nao kwa wema sana.

April fool na Uislam


Sitaki kuzungumzia asili ya April Fool day ili kufupisha mada yangu. Kila mmoja akae atafute asili ya April fool ni ipi basi muislamu wa kweli hakika hatokuwa pamoja na waongo na atajiepusha na kusema UONGO.

Ninachotaka kukizungumzia hapa ni hichi kitendo cha waislamu kusema Uongo kila ikifika tarehe mosi April. Uongo ni haramu haramu tena ni haramu. Na kuna makatazo makubwa ndani ya uislamu kuhusu Uongo. Leo muislamu anasema uongo kumwambia mwenzake je hakai akafikiria kuwa anaweza kumsababishia muislamu mwenzake kupata madhara? 

Leo unamwambia mtu aende sehemu kuna ajali au lolote je unajua mwenzako yuko katika hali gani wakati unampa habari hiyo? Halafu muislamu anacheka na kujidai kuwa amempata siku ya wajinga.

Mtume(swalla Allahu alayhi wasallam)anasema"Uongo ni haramu japokuwa ni maskhara"Katika jambo la kusema uongo waislamu tumekatazwa na tumetakiwa tuwe nalo mbali kabisa na kuna maonyo makali kutoka kwa Mtume (swalla Allahu alayhi wasallam). Kutoka kwa Muaawiyah bin Haydah Amesema: " Nimemsikia Mtume Swalla Allaahu alayhi wasallam akisema:"Ole wake kwa anayehadithia jambo la uongo ili watu wacheke. Basi ole wake! Ole wake! (At-Tirmidhiy na amesema hii ni Hadiyth Hasan, na pia imepokelewa na Abu Daawuud)

JE VIPI MTUME (SWALLA ALLAHU ALAYHI WASALLAM) ALIKUWA AKIFANYA MZAHA

Kutoka kwa Ibn Umar (Radhiya Allaahu anhuma) ambaye amesema: Mtume (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika mimi nafanya mzaha lakini sisemi ila tu yaliyo ya kweli" Attwabarany

Na tukumbuke kuwa miongoni mwa alama za mnafik moja wapo anapozungumza basi husema uongo. Imetoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Alama za munaafiq ni tatu; akizungumza husema uongo, akitoa ahadi huivunja, akiaminishwa kwa kitu hufanya khiyana" Al-Bukhaariy na Muslim.

Ndugu zangu wa kiislamu tujiepusheni na jambo hili la kusema Uongo na tuwe wenye kuwakataza na wenzetu. Na mtu anaweza kusema nitatubia lakini mara hii lazima nimpate au hii mara ya mwisho. Basi wewe waza katika akili yako na je wakati unasema uongo malaika wa kutoa roho anakuja kuchukua roho yako na hujatubia. Nini utamjibu Allah wakati umerudi kwake unasema Uongo?

ALLAH ATUJAALIE WALE WENYE KUAMBIWA MAZURI NA KUYAFANYIA KAZI NA KUKATAZWA MABAYA NA KUYAWACHA"Aaamin.

“NA KUMBUSHA, KWANI UKUMBUSHO HUWAFAA WAUMINI”(51:55).

Siri ya maisha


Huenda wengine wakakuona msafi, na huenda wengine wakakuona muovu, na huenda wengine wakakuona.......

Lakini siri ya pekee ambayo haijui mwengine ila wewe ni: 

siri ya mafungamano yako na Mungu wako

Basi wasikughuri wanaokusifu... wala wasikudhuru wanaokukejeli.......

Mwenyezi Mungu amesema: 

{Bali mtu ni shahidi juu ya nafsi yake}.

(Suratul Qiyama : 14)

Wasia tisa


Wasia tisa kutoka Quran (Suratul Hujurat) za kutufunza kudili (kuamiliana) na watu: 

1- Chunguzeni kwanza ukweli wa habari (mnapoletewa habari). 

2- Fanyeni suluhu (patanisheni baina ya watu waliogombana). 

3- Hukumuni kwa haki. 

4- Msiwadharau watu. 

5- Msitukanane kwa makabila. 

6- Msiitane kwa majina mabaya. 

7- Jiepusheni sana na kuwadhania watu dhana mbaya. 

8- Msipeleleze habari za watu. 

9- Msisengenyane

zihifadhi vizuri na uzichunge maishani. 

si jukumu lako kumfurahisha kila mtu lakini ni jukumu lako kutomuudhi mtu. 

Zingatio kwa kila mwenye mke


Daima jaribu uwezavyo kuwa mtu mzuri kwa mkeo kwa njia ya maneno na vitendo. Ongea nae, mchekee, tafuta ushauri wake, muulize juu ya mawazo yake, tumia-wakati maalum na yeye na daima kumbuka kwamba Mtume Mohammed (s.a.w) alisema:-((Wabora katika nyinyi ni wale ambao ni wabora kwa wake zao))

Ushauri muhimu kwa wote


Madamu moyo wako bado unapiga, usipoteze mambo matatu:

-Imani yako kwa Mungu
-Tumaini lako kwa Mungu
-Tegemeo lako kwa Mungu

Tunafanya mambo tunavyotaka sisi, bila kuangalia wapi Mungu katoa na wapi kaharamisha, na wapi kafaradhisha...Ewe Mungu wetu tunajikinga kwako na shida mbili: (mandhari mabaya na mabadiliko mabaya). 

Huenda mauti yapo karibu nasi na hatuhisi,huenda yanakumbatia pumzi zetu kila sekunde nasi tumeghafilika! Ewe Mungu tupe nafuu wakati wa kutolewa roho na tupe mwisho mwema. 

Usiamini sana, usipende sana, usitumai sana,kwani mno itakuumiza sana. 

Toa nasaha na usifedhehi, na laumu bila kujeruhi. 

Hakuna budi kuwepo na kukinai (kuridhika) kikweli kweli kwamba tuliyoandikiwa tutayapata hata kama hatuyataki...na tusiyoandikiwa hatutayapata hata kama tutayapigania hadi kifo. 

Pale nia zinapokua safi, matamanio yetu tutayafikia. 

Mimi ni Muislamu, na Uislamu ni dini kamili; lakini mimi ni binadamu si mkamilifu..
kwa hiyo nikifanya makosa musilaumu Uislamu bali nilaumuni mimi. 

Heshima ni malezi si udhaifu, na kuomba radhi ni tabia si madhila

Usihuzunike asipothamini mtu juhudi na wema wako, kwani tabia ya watu hawadiriki neema ila baada ya kuwatoka

Ewe Mungu tupe woga ili utuzuie na kukuasi, na tupe uchamungu ili itufikishe peponi mwako, na tupe yakini ili ituwepesishie Maafa ya dunia...

Nasaha Muhimu


Anza siku yako kwa kumtaja na kumkumbuka Mungu katika nyakati za asubuhi upate kufaulu.

Endelea na kuomba msamaha kwa Mungu mpaka shetani akaribie kujiua.

Usiache dua kwani ndio kamba ya uokofu.

Kumbuka maneno yako yanaandikwa na malaika.

Kua na matarajio mema hata kama uko katika kidimbwi cha kimbunga (matatizo).

Uzuri wa vidole ni kuvifungamanisha na tasbih.

Wasiwasi na dhiki zikizidi sema: "LAA ILAHA ILLA ALLAH."

Nunua dua ya fakiri na mapenzi ya maskini kwa pesa.

Sijda ndefu kwa ajili ya Mungu yenye unyenyekevu ni bora kuliko makasri mazuri (Majumba ya kifakhari).

Fikiri kabla hujatoa neno kwani huenda neno likaua.

Jihadhari na dua ya madhlum na chozi la mwenye kunyimwa (maskini).

Kabla kusoma vitabu na magazeti: soma 
Qur-an.

Tengeza sababu ya kunyooka watu wako.

Jitahidi nafsi yako katika utiifu kwani nafsi ni yenye kuamrisha maovu sana.

Busu viganja vya wazazi wako utapata radhi.

Nguo zako kuukuu ni mpya kwa mafukara.

Usighadhibike (usikasirike) maisha ni mafupi kuliko unavyodhania.

Uko na mwenye nguvu wa wenye nguvu na tajiri wa matajiri naye ni Mungu Aliyetukuka.

Wingi wa kutoka kwako pasi na haja ni inadi na uovu.

Usifunge mlango wa kabuli kwa maasi.

Sala ni kitu bora cha kukusaidia kwenye misiba na machofu.

Jiepushe na dhana mbaya utapumzisha watu na utapumzika wewe mwenyewe pia.

Sababu ya kila dhiki ni kumpa nyongo Mungu basi mkabili (muendee).

Sali sala utakayoingia nayo kaburini mwako.

Ukimsikia asi anasengenya mwambie: mche Mwenyezi Mungu.

Dumu katika kusoma surat Tabaraka kwani inaokoa.

Mwenye kunyimwa (maskini) ni aliyenyimwa sala ya unyenyekevu na jicho la kutoa machozi.

Usimuudhi muumini.

Fanya mapenzi yako yote kwa Mungu na Mitume wake saw.

Msamehe aliyekusengenya kwani amekupa thawabu zake.

sala, kusoma Qur-an na kumkumbuka Mungu ni mafungamano ya kunawiri kifuani mwako.

Anayekumbuka joto la moto anasubiria sababu za maasi.

Madamu usiku hupita basi uchungu utaondoka, na matatizo yatatatuka na shida itapita.

Epuka kusengenya (qiila wa qaala: alisema, kulisemwa)kwani una amali kama majabali.

Sali kwa unyenyekevu kwani yote yanayokusubiri si muhimu kuliko sala.

Weke Qur-an kichwani kwako kwani kuisoma aya moja ni bora kuliko dunia na vilivyomo ndani yake.

Maisha ni mazuri na kizuri zaidi ni wewe kwa imani yako na tabia yako na heshima yako.

Zingatia haya yatakusaidia katika maisha yako..

Kitu kizuri na chenye manufaa duniani ni kuilea nafsi iwe yenye kuridhika na kushukuru, na kuwa na nia safi.

Na hakuna kitu chema chenye kuleta faida kama kuwasamehe WENZAKO wote wenye kukukosea na wenye kukuchukia!

Lakin kuna jambo jingine bora zaidi hata Mtume
(S.A.W.) aliwahi kumuusia mmoja kati ya swahaba wake zaidi ya mara 3,
na kila mara alirudia akisistiza:

"USIKASIRIKE!"
"USIKASIRIKE!"
"USIKASIRIKE!"

Kwani hasira huzaa Chuki,
Chuki huzaa maudhi,
Maudhi huzaa kisirani, na
Kisirani huondosha nuru njema maishani na
huondosha mapenzi, maelewano, utulivu, na amani.

Tuazimie kutenda mema na Mungu Atatujaalia tawfiq,

In Sha Allah

Tuamrishane mema

Mtoto alimuomba mamake amueleze kwa ufupi ujuzi wake na hikma alopata maishani, mamake akwambia: "utaweza kusikiliza?"

Akajibu: ndio......

Mama akasema:

Mwanangu: jichunge na kuzungumzia watu au mambo hadi uhakikishe ukweli wake, na akikujia mtu na habari yoyote hakikisha kabla kukimbilia......!

Na jihadhari na uvumi
Usiamini kila linalosemwa, wala nusu ya unayoyaona, na Allah akikuonja kwa adui pambana naye kwa kumfanyia hisani... sukuma uovu wake kwa lililo jema, nakuapia kwa Allah uadui utageuka mapenzi...

Ukitaka kumjua undani rafiki; safiri naye!
Safarini mtu hudhihirika uhakika wa undani wake....

Watu wakikuhujuma nawe uko kwenye haki furahia; kwasababu ni kama wanasema wewe umefaulu na unaathiri, kwani mbwa akiyekufa hapigwi teke, na haupurwi ila mti unaozaa matunda....!!

Mwanangu: ukitaka kuchagua mtu... mtazame kwa jicho la nyuki na usitazame watu kwa jicho la nzi kuangalia ubaya tu ulipo!

Lala mapema mwanangu kwani baraka ya rizki ni asubuhi, nakuhofia uikose riziki ya Allah Alrahman kwa kuwa unakesha....

Na nitakuhadithia kisa cha mbuzi na mbwa mwitu ili usimuamini anayefanya hila. Na mtu akikuamini, basi chunga tena chunga usimkhuni.....!

Nitakupeleka kwenye nyumba ya simba nikuoneshe kuwa simba hakuwa mfalme wa msitu kwa kuwa ananguruma ! Lakini ni kwasababu yeye ana ezi ya nafsi, hali windo la mwenzake hata akawa na njaa sana, basi usiibe juhudi ya mwenzako ukawa dhalimu....!!

Nitakupeleka kwa kinyonga, ili uone mwenyewe hila zake.! Anajigeuza rangi kwa rangi ya sehemu aliyo, ujue katika watu pia kuna mfano wake.....!!

Jizoeshe kushukuru mwanangu.......
Mshukuru Mwenyezi Mungu inatosha kuwa wewe ni Muislamu, inatosha kuwa unatembea, unasikia, unaona,,,,,,,,,,, mshukuru Mwenyezi Mungu na uwashukuru watu.. Mwenyezi Mungu anawazidishia wenye shukrani.. na watu wanapenda wakimpa mtu ashukuru.

Sifa njema kubwa katika maisha ni UKWELI.... na jua kwamba uongo hata ukiokoa ni muovu kabisa katika sifa mbovu...

Mwanangu.... jiwekee badala ya kila kitu, jitayarishe kwa jambo lolote, ili usidhalilike na kudharaulika.

Na ufaidike na fursa yoyote unayoipata sasa, huenda usiipate tena.

Usilalamike wala usijidhalilishe !! Nataka uwe mwenye hisia chanya uyakabili maisha, wakimbie wanaokata tamaa na wenye hisia hasi... na jihadhari kukaa na mtu anayepiga bao...!!

Usifurahie msiba wa mwenzako, na jihadhari na kumdharau mtu kwa umbo lake, kwani hakuna aliyejiumba.! Na katika kufanya dharau unakuwa unamfanyie aliye umba.

Kwa mafunzo na faida.... matatu:

-Usichukue vitu vitatu mpaka uviulizie:
Asali, dini, na mke.

-na vitatu hutapumzika hadi vikuepuke:
Wasiwasi, deni, na rafiki muovu.

- na vitatu vikichelewa vinakuwa havina faida:
Walima, taaziya na sala ya maghrib.

- na watatu Mungu akulinde nao:
Mwana wa haramu, mkata kizazi, na mla riziki ya mayatima.

-na watatu jiepushe na kuandamana nao:
Aso na akili, aso jali, aso na utu.

-na watatu usiwasikize:
Muongo, mfitinishaji, na mtoa ushuhuda wa uongo.

-na watatu usiwafanye marafiki:
Hasidi, na mwenye kijicho, na mwenye kukasirisha wazazi.

-na watatu usivunje rai zao:
Mwenye kuhifadhi sala yake, na mkarimu, na mwenye kuridhisha wazazi.

TUAMRISHANE MEMA

Zingatia haya

Ndugu zangu wapendwa,

Hisani yako na utangamano wako hausahauliki, usijute kwa madakika uliyomfurahisha mtu katika maisha yake hata kama alikuwa hastahiki kufanyiwa hivyo...! Kuwa kitu kizuri katika maisha ya kila anayekujua.

Inatutosha kuwa tuna Mungu anatulipa wema kwa wema....!!!

Maisha yetu ni karatasi

Cheti cha kuzaliwa ni .....karatasi

Cheti cha chanjo ni
.....karatasi

Cheti cha kufaulu ni
..... karatasi
Cheti cha kuhitimu ni
....karatasi

....karatasi zinafatia.....

Cheti cha ndoa...karatasi

Pasi ya kusafiri...karatasi

Hati miliki ya nyumba...
Karatasi

Cheti cha tabia njema...
Karatasi

Wasifa ya matibabu...
Karatasi

Ualishi wa shughuli....
Karatasi

Maisha yetu ni karatasi kwenye karatasi......
Zinakunjwa na siku..na kupasuliwa...kisha dunia inazitupa zote...karatasi........

Mwanadamu mara ngapi anahuzunika..kwa karatasi, na kufurahika......kwa karatasi..
Lakini.........

Karatasi ya pekee ambayo mwanadamu hawezi kuiona ni:
Karatasi ya cheti cha kufariki....

Ifanyie kazi kwani ndio karatasi muhimu..!

Mkono kwa mkono hadi peponi.

Nyiradi za asubuhi na jioni

Application ya simu ‘Nyiradi za asubuhi na jioni na dua za Quran na maana yake kwa kiswahili' 

https://play.google.com/store/apps/d...m.Asmi.nyiradi

Yasome haya yatakusaidia katika maisha yako

Mueke chura kwenye kiti cha dhahabu utamuona ataruka aende kwenye tope hivi ndio baadhi ya watu walivyo, namna utakavyomuenua atarudi mahala anapotoka....

Usimhuzunikie mtu aliyekubadilikia ghafla, huenda ikawa ameacha kujifanyisha.. (pretend)

Mwenyezi Mungu amewaumba malaika wana akili bila ya matamanio, na akawaumba wanyama wana matamanio bila akili, na akamuumba mwanadamu akampa akili na matamanio, basi ambaye akili yake itashinda matamanio yake anaungana na malaika, na ambaye matamanio yake yatashinda akili yake anaungana na wanyama.

Mwanadamu maishani ni kama kalamu (pencil), anachongwa na makosa ili aandike kwa khati nzuri..anaendelea hivi mpaka kalamu iishe na kunabaki mazuri aloyaandika.

Usililie kila kitu kilichopita na iwe ni funzo kwako, hakuna kitu kinakufanya mkubwa isipokuwa maumivu makubwa, na sio kila kuanguka ndio mwisho kwani kuanguka kwa mvua ni mwanzo mwema.

Uslubu wako ni fani: kutangamana na wengine ndio cheo chako, kila uslubu wako ukipanda cheo chako kinapanda.

Wanamsifu mbwa mwitu naye ni hatari kwao, na wanamdharau mbwa naye ni mlinzi wao...watu wengi wanawadharau wanaowahudumia na wanawaheshimu wenye kuwadharau.

Kuwa na mnyama rafiki ni bora kuliko kuwa na rafiki mnyama!!

Nilitabasamu nilipokosa ninachokitaka nikafahamu kuwa Mungu anataka nipate zaidi ya ninachotaka nikatabasamu tena upya...

Ukiumia kwa maumivu ya mwengine basi wewe ni mwema, na ukishiriki katika matibabu yake, basi wewe ni mtukufu...

Huyu ndio "Shetani"

Je unaijua Kazi yake katika jamii?

"Hapendi kuona AMANI katika Ndoa",
Hataki kuona UKISALI",
Anapenda kukuona ukitafuta "PESA" Bila kuridhika!"

Je unajua anapoishi?
Sehemu anayopenda ni pale ambapo hakuna jina la Allah (sehemu ambayo hatajwi Mwenyezi Mungu)!

Vipi unawafahamu rafiki zake?

Rafiki zake wakubwa ni...!
WAZINZI, WEZI, WALEVI, WANAFIKI, WAONGO, WALA RIBA, WASIO HESHIMU WAZAZI, WASIO SWALI, na WAFITINISHAJI.

JE unaijua fimbo yake ya kumpigia?

Wewe sema AUDHUBILLAH MINASHAYTWAANRAJIIM! (Najikinga kwa Mwenyezi Mungu anilinde na Shetani)
Au wewe mtaje , MUNGU kila mara mfano, uwe unasema ALLAH AKBAR (Mungu Mkubwa kuliko kila kitu), N.K

Mimi nimefikisha ujumbe kwako je wewe unamfikishia nani?

Tupunguzeni israfu na tuwasaidie maskini

Ni mara ngapi unafanya israfu ya chakula?

Ni mara ngapi unakitupa chakula kilichobaki kwa kuwa hamkitaki wala hakijaharibika?

Ni mara ngapi ni mwenye kuwalisha wenye nacho na kuwasahau maskini na mafukara wenye kulala na njaa?

Watoto wangapi wanakufaa kwa sababu ya njaa?

Tuko wapi Ummat Muhammad? Kwa nini usijipangie kawaida ya kutoa kwa kuwa unacho au kila pale utakapopata?

Nyoyo zimejaa tamaa hatutosheki na tunavyoruzukiwa. Muislamu anatupa nguo hali ya kuwa jirani yake hana cha kuvaa au muislamu mwenzake nchi za kimaskini hana cha kukivaa?

Tukumbuke hizo ni neema kwa Allah na tutakuja kuulizwa. Au tunasubiri watokezee wakristo ndio waje kuwasaidia waislamu ?

Sayyidina Othmaan alitoa sadaka ya msafar mzima wa biashara yake kwa waislamu wenye njaa. Hivi muislamu anaweza kusema hatonunua nguo kwa sababu anazo nyingi bali atoe sadaka?

au atatamani na yeye anunue ili azidi kujifakhirisha?

Ukifa unaenda na sanda tu huendi na viatu vyako wala nguo zako tanguliza mema kwa ajili ya maisha ya akhera. Mwanamke anaweka kanga zinafika pea 100 au mwanamme anaweka kanzu au nguo nyengine tele wallah kuna watu wanahitaji mvao mmoja au nguo moja tu ili ajistiri na mjuislamu anayajua ila moyo wake haushtuki. Raha yake ajaze nguo kabatini.

Subhana Allah wapi tunakwenda enyi waislamu?

Kwa nini tusikae tukawaza mambo ya kheri?

Tufanyeni haya kwa ajili ya Allah na si kujionesha.

Tukumbukeni aya za Allah zifuatazo :

"Tena bila ya shaka mtaulizwa siku hiyo juu ya neema." (8:102)

"Ogopeni Siku Ambayo Mutarudishwa Kwa Allah Kisha Kila Nafsi Italipa Kila Lile Ililochuma Na Wao Hawatadhulumiwa"(2:281)

Mtume Muhammad s.a.w anatwambia katika hadith refu ilopokelewa na Imamu Muslim, kua mja ataambiwa na Allah "Ewe mja wangu nilikutaka unilishe lakini hukunilisha, Mja atasema vipi nitakulisha hali ya kua wewe ndie Mola wa viumbe vyote?

Allah atamuambia;Jee hukujua kua mja fulani alihitaji umlishe lakini hukumlisha? Jee hujajua kama ungelimlisha basi ungelilikuta hilo kwangu?"

Nitakutumieni video yenye kutoa chozi juu ya misiba iliyowahi kuwakuta somalia. Halafu tuseme na nafsi zetu juu ya hali hizo.

Zingatia haya na yatumie katika maisha yako yatakusaidia

"Mtu aliyezama kwenye mapenzi ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka,,,,,,,,

,,,,, namna anavyo chapwa na mitihani ndivyo anavyozidi mapenzi na kujikaribisha kwa Mungu"

Ameangamia kila anayeadhibu na kukhini na kudharau hisia za mwanadamu, hajui kuwa katika ulimwengu huu.... unavyowatendea watu ndivyo utakavyolipwa.

Ni uzuri ulioje uvae tabia njema zako.... na ujitie manukato ya tabasamu lako.. hata yanapokua.. mandhari (shepu) yako.... ni ya kiajabu na kutofahamika kwa wengine.... utakuta kizuizi hiki kinafifia na utafurahia.......

Mke hana haja ya.....
matumizi na maskani (nyumba) peke yake.... lakini pia... anahitaji maneno mazuri, moyo mzuri, mapenzi.. na huruma... mhurumie mke wako na msahaulishe mchoko wake......

Baadhi ya watu, ukiwaheshimu,.... wanazidisha kukutendea uovu,.... (wewe usijali usiaje kuwa mwadilifu)

Urafiki mwema: ni ule..... unaokufanya ukaishi maisha mawili...,

moja hapa... ingine .... peponi.........


Kujiheshimu..., heshima sio katika mavazi peke yake.... bali kuna kicheko...cha kuheshimika... mwendo wa kuheshimika..... na tabia za kuheshimika..........

Usimuache mtu mpenzi (muhimu) kwako kwasababu ya kosa (kuteleza).....au ila aliyonayo.... hakuna aliye kamili... isipokuwa Mwenyezi Mungu... Utukufu ni wake Yeye tu......

Katika matatizo ya watu....wanaweza kufuta... historia yako nzuri yote.... kwa ajili ya msimamo wa mwisho ambao haukuwapendeza.....

Uzuri hauna thamani.......bila fikra...na maadili mema....na tabia.

Haupimwi utamu wa mwanadamu...kwa utamu wa ulimi.... ni maneno mangapi mazuri...yameficha sumu ya nyoka..... kwani tupo katika wakati... mambo yamevurugika...

Peaneni msamaha.... na muzifanye nyoyo zenu nyeupe..... na kumbukeni kuna siku...... hatutakuwa katika maisha haya....

Vitu vyote vinaenda havirudi..... isipokuwa dua.....inaenda na matumaini: ....na inarudi [na zawadi].

Maneno ni kama dawa.... machache yake yanufaisha ..... na mengi yanaua....

Urafiki si....kubaki na rafiki...muda mrefu..., .........urafiki ni kudumu ...... kwenye ahadi ikiwa....ni masafa marefu au mafupi....

Katika ajabu ya mwabaadamu...anakimbia anaposikia (nasaha) na anaskiza anaposikia (fedheha)

Kuna watu wanahitaji ........ urekebishaji wa kupambwa kindani.... kukuzwa moyo, ... kuondolewa chuki..... kukazanishwa ulegevu wao wa fikra..., kuvunjwa chembe chembe (cells) za shari kwenye nafsi zao..... na kupulizwa dhamiri zao dhaifu.....


Ulimi ni mhalifu!.... mfungwa nyuma ya meno!.... ukiufungua wakati wa hasira... utakutupa kwenye kipango cha majuto ".....
...... chini ya hukumu.... ya dhamiri !

Hebu jiulize masuala haya.....

HEBU jiulize masuala haya na lifikirie katika akili yako kila suala jibu utapata mwenyewe 
Mimi ni nani katika hii dunia?

Nimeishi miaka mingapi hadi sasa?

Nimebakiza miaka mingapi ya kuishi?

Nimefanya mangapi kwa ajili ya akhera yangu?

Maovu mangapi nimetenda kwa kuteleza au kwa makusudi?

Lini nilitoa chozi kutubu mabaya yangu? 

Lini nilikaa faragha na kumshukuru M/Mungu kwa wema anaonitendea? 

Hivi Mungu akichukua roho yangu wakati huu, nimebeba kazi (amali) ngapi za kheri zitakazo nisaidia?.

Nitakumbukwa kwa wema gani niliowatendea wanadamu na viumbe wengine?

ZINDUKA NDUGU YANGU.DUNIA ISITUHADAE TUKAMSAHAU MUNGU. Wakumbushe na wengine.