Thursday 10 July 2014

Ushauri muhimu kwa wote


Madamu moyo wako bado unapiga, usipoteze mambo matatu:

-Imani yako kwa Mungu
-Tumaini lako kwa Mungu
-Tegemeo lako kwa Mungu

Tunafanya mambo tunavyotaka sisi, bila kuangalia wapi Mungu katoa na wapi kaharamisha, na wapi kafaradhisha...Ewe Mungu wetu tunajikinga kwako na shida mbili: (mandhari mabaya na mabadiliko mabaya). 

Huenda mauti yapo karibu nasi na hatuhisi,huenda yanakumbatia pumzi zetu kila sekunde nasi tumeghafilika! Ewe Mungu tupe nafuu wakati wa kutolewa roho na tupe mwisho mwema. 

Usiamini sana, usipende sana, usitumai sana,kwani mno itakuumiza sana. 

Toa nasaha na usifedhehi, na laumu bila kujeruhi. 

Hakuna budi kuwepo na kukinai (kuridhika) kikweli kweli kwamba tuliyoandikiwa tutayapata hata kama hatuyataki...na tusiyoandikiwa hatutayapata hata kama tutayapigania hadi kifo. 

Pale nia zinapokua safi, matamanio yetu tutayafikia. 

Mimi ni Muislamu, na Uislamu ni dini kamili; lakini mimi ni binadamu si mkamilifu..
kwa hiyo nikifanya makosa musilaumu Uislamu bali nilaumuni mimi. 

Heshima ni malezi si udhaifu, na kuomba radhi ni tabia si madhila

Usihuzunike asipothamini mtu juhudi na wema wako, kwani tabia ya watu hawadiriki neema ila baada ya kuwatoka

Ewe Mungu tupe woga ili utuzuie na kukuasi, na tupe uchamungu ili itufikishe peponi mwako, na tupe yakini ili ituwepesishie Maafa ya dunia...

No comments:

Post a Comment