Thursday 10 July 2014

Hakika Halali Iko Wazi Na Haramu Iko Wazi


Kutoka kwa- Abu Abdullah An-Nu’uman Ibn Bashiyr -(RA) -ambaye alisema: Nilimsikia Mtume Mohammad (SAW) akisema:

Halali iko wazi na haramu iko wazi, baina yao ni vitu vyenye shaka ambavyo watu wengi hawajui.-- Kwa hivyo, yule anayeepuka vyenye shaka- anajisafisha nafsi yake kwenye dini yake na heshima yake, lakini yule anayetumbukia katika mambo yenye shaka, huanguka katika haramu, kama mchungaji anayechunga (wanyama) pembezoni mwa mpaka, mara- huingia ndani (ya shamba la mtu).- Hakika kila mfalme ana mipaka yake, na mipaka ya Mwenyezi Mungu ni makatazo Yake. Na hakika katika kiwiliwili kuna kipande cha nyama kikitangamaa, kiwiliwili chote hutangamaa, na kikharibika kiwiliwili chote huharibika. Basi jua (kipande hicho cha nyama) ni moyo.

Imesimuliwa na Al-Bukhari na Muslim

1 comment: