Thursday 10 July 2014

Wasia wa Luqman Kwa Mwanae (Na kwetu sisi sote)


Assalam Alaykum Warahmatullah Wabarakatuh;

Katika makala hii fupi, utapata ingawa kwa ufupi wasia alioutowa luqman kwa mwanae. Kwa hikma ya kisa hiki cha mja huyu mwema ndani ya Qur’an ni kwa malengo yetu sote na pili umuhimu wetu kuwa nasihi watoto wetu katika ibada.

Katika nasaha alizompatia mwanawe ni kuwatendea wema wazazi, kutokua na kibri, kusimamisha Swalah, kuamrisha mema na kukataza maovu, kusubiri, kutonyanyua sauti na kadhalika kama Alivyotupa maelezo hayo Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):

‘Ewe mwanangu! Kikiwapo kitu cha uzito wa chembe ya khardali kikawa ndani ya jabali au ndani ya mbingu au ndani ya ardhi, basi Allaah Atakileta. Hakika Allaah ni Mjuzi wa yaliyofichika, Mwenye khabari za yote’. -

‘Ewe mwanangu! Shika Swalah, na amrisha mema, na kataza maovu, na subiri kwa yanayo kupata. Hayo ni katika mambo ya kuazimiwa’

‘Wala usiwabeuwe watu, wala usitembee katika nchi kwa maringo. Hakika Allaah Hampendi kila anayejivuna na kujifakhirisha‘ [Luqmaan:16-18]
Mahmoud Al-Asmi at 18:30

No comments:

Post a Comment