Tuesday 19 August 2014

Zingatia haya yatakusaidia

Kuachana na swala inamaanisha kwamba utakosa raha ya nafsi katika dunia hii..amesema Mwenyezi Mungu: Na anayepingana na utajo wangu hakika atapata maisha ya dhiki

Hao ni wenye matumaini wale wanaoshibisha roho yako tamaa na kukusukuma kufanya kazi, wanakuliwaza kwa hekima kutokana na mateso yako na wanayapoza, na wanairutubisha furaha yako na wanatia nguvu ndoto yako na wanaiamsha..hao wafanye marafiki

Kama unataka kugeuza nafsi yako na kuipaisha kwa kiwango bora, huna budi utambue kwamba hatua ya kwanza ya mageuzi inatoka ndani yako... mageuzi yanaanza kwa nia ya mageuzi

Juu yenu kutubu.. kwani ina faida kwenu kuliko faida ya upanga
-alfudhail bin 'ayyaadh

Kuwa mtu mwema kwa unaowapita wakati unapanda kileleni.. kwani utakutana nao wakati unateremka! hakuna mmoja anayebaki kileleni maisha yote
  -steven cofey

Mtume Muhammad SAW alikusanya baina ya taqwa na tabia njema, kwani kumcha Mwenyezi Mungu ni baina ya mja na Mola wake, na tabia njema ni baina yake na viumbe
   -ibn alqayyim

(watapambwa kwa bangili za dhahabu) peponi; mapambo kwa wote, wanaume na wanawake..ni peponi.. huko kuna vinavyotamanisha nafsi na kuburudisha macho na kayafurahisha

Imepokewa na Jarir bin Abdallah amesema: Amesema Mtume SAW:

Amesema Mtume Muhammad SAW: hakika salaam (amani) ni jina miongoni mwa majina ya Allah SW lililowekwa kwenye ardhi, basi enezeni salamu baina yenu>>

Amiliana kwa wema kwa anayestahiki na asiyestahiki, kwani wewe unatafuta nyumba ya peponi si nyumba kwenye moyo wa kila mtu

Izoeshe nafsi yako kwenye mambo matatu:
- ukifanya jambo kumbuka Mola anakuona,
-na ukiongea ujue Mola amekusikia,
-na ukinyamaza elewa kwamba Mola anajua unachofikiri
  -hatim al asam

Wanadamu ni watu wa ajabu.. wanatenda kwa ajili ya dunia, huku wakiruzukiwa bila  amali..na wala hawafanyi kwa ajili ya akhera, ambapo hawataruzukiwa ila kwa amali

Kuchora tabasamu ni jambo jepesi ambalo unalifanya na kwa ujira mkubwa

Kila kitu inawezekana kukinunua ila nia nzuri, hiyo chimbuko lake linatoka kwenye kisima cha kichawi ndani ya nyoyo safi

Kila starehe isiyokuwa kwa ajili ya Allah, itabadilika na kuwa majuto kwa aliyeifanya siku ambayo ukubwa wake ni miaka elfu hamsini! mwenye akili ni yule anayestarehe mara mbili.. hapa duniani kwa twaa ya Mwenyezi Mungu, kisha peponi

Jiondoshee hisia za mateso, na mateso yenyewe yataondoka
-marcus aurelios

Mvivu hahisi thamani ya raha, kinyume na mchapa kazi ambaye anifurahia baada kufanya juhudi, akitaka kurudisha nguvu zake

Ewe Mola waponye wagonjwa waislamu, na walishe wenye njaa, na warudishe waliopotea, na waachie huru wafungwa wao, na warehemu maiti wao, na wape usalama na amani popote walipo katika ardhi hii ewe Mola wa viumbe vyote

       

No comments:

Post a Comment