Thursday 10 July 2014

Kuwadanganya wanawake


Mmoja wa wenye hikma alisema: 
Jihadhari na kuwadanganya wanawake, kwani wana uhodari wa kujua ukweli, na uwezo mkubwa wa kujifanya hawajajua...!

"Mwenye kupoteza penzi la mwanamke muaminifu, amepoteza maisha yake yote"

- Je unajua kwamba......

1- mwanamke akiwasiliana nawe sana inamaanisha hataki kuongea na mwengine..?

2- mwanamke atapata mwanamme bora kuliko wewe kwasababu amejifunza kuchagua kwa jeraha lake.....

3- mwanamke aliyedhulumiwa, mwanamme atamrudia wakati akiwa ameshachelewa... (too late..!!)

4- mwanamke anamiliki hisia ya sita zaidi ya mwanamme kumjua akibadilika au akimkhuni.......!

5- mwanamke anasubiri na kuvumilia sana kuliko mwanamume.. na akimuacha mwanamme basi ni baada ya kujaribu kumuomba msamaha mara elfu..

6- mara nyingi mwanamke akiungulika anapendelea kunyamaza.....

7- mwanamke anaporeact na kukulaumu hii inamaanisha mapenzi yake mingi kwako...

8- mwanamke anapokua amekerwa na mwanamme ananyamaza kwa kutaraji kuwa atabadilika na sio kwa kutojua....

9- mwanamke akizungumziwa na mwanamme kuhusu mwanamke mwengine, huficha kilio chake nyuma ya tabasamu lake......

Mtume Mohammed (saw) kamfananisha mwanamke na chupa ya kiyoo tuibebe pole pole isituponyoke ikavunjika

Na maana yake tuishi nao kwa wema sana.

No comments:

Post a Comment