Thursday 10 July 2014

Zingatia haya na yatumie katika maisha yako yatakusaidia

"Mtu aliyezama kwenye mapenzi ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka,,,,,,,,

,,,,, namna anavyo chapwa na mitihani ndivyo anavyozidi mapenzi na kujikaribisha kwa Mungu"

Ameangamia kila anayeadhibu na kukhini na kudharau hisia za mwanadamu, hajui kuwa katika ulimwengu huu.... unavyowatendea watu ndivyo utakavyolipwa.

Ni uzuri ulioje uvae tabia njema zako.... na ujitie manukato ya tabasamu lako.. hata yanapokua.. mandhari (shepu) yako.... ni ya kiajabu na kutofahamika kwa wengine.... utakuta kizuizi hiki kinafifia na utafurahia.......

Mke hana haja ya.....
matumizi na maskani (nyumba) peke yake.... lakini pia... anahitaji maneno mazuri, moyo mzuri, mapenzi.. na huruma... mhurumie mke wako na msahaulishe mchoko wake......

Baadhi ya watu, ukiwaheshimu,.... wanazidisha kukutendea uovu,.... (wewe usijali usiaje kuwa mwadilifu)

Urafiki mwema: ni ule..... unaokufanya ukaishi maisha mawili...,

moja hapa... ingine .... peponi.........


Kujiheshimu..., heshima sio katika mavazi peke yake.... bali kuna kicheko...cha kuheshimika... mwendo wa kuheshimika..... na tabia za kuheshimika..........

Usimuache mtu mpenzi (muhimu) kwako kwasababu ya kosa (kuteleza).....au ila aliyonayo.... hakuna aliye kamili... isipokuwa Mwenyezi Mungu... Utukufu ni wake Yeye tu......

Katika matatizo ya watu....wanaweza kufuta... historia yako nzuri yote.... kwa ajili ya msimamo wa mwisho ambao haukuwapendeza.....

Uzuri hauna thamani.......bila fikra...na maadili mema....na tabia.

Haupimwi utamu wa mwanadamu...kwa utamu wa ulimi.... ni maneno mangapi mazuri...yameficha sumu ya nyoka..... kwani tupo katika wakati... mambo yamevurugika...

Peaneni msamaha.... na muzifanye nyoyo zenu nyeupe..... na kumbukeni kuna siku...... hatutakuwa katika maisha haya....

Vitu vyote vinaenda havirudi..... isipokuwa dua.....inaenda na matumaini: ....na inarudi [na zawadi].

Maneno ni kama dawa.... machache yake yanufaisha ..... na mengi yanaua....

Urafiki si....kubaki na rafiki...muda mrefu..., .........urafiki ni kudumu ...... kwenye ahadi ikiwa....ni masafa marefu au mafupi....

Katika ajabu ya mwabaadamu...anakimbia anaposikia (nasaha) na anaskiza anaposikia (fedheha)

Kuna watu wanahitaji ........ urekebishaji wa kupambwa kindani.... kukuzwa moyo, ... kuondolewa chuki..... kukazanishwa ulegevu wao wa fikra..., kuvunjwa chembe chembe (cells) za shari kwenye nafsi zao..... na kupulizwa dhamiri zao dhaifu.....


Ulimi ni mhalifu!.... mfungwa nyuma ya meno!.... ukiufungua wakati wa hasira... utakutupa kwenye kipango cha majuto ".....
...... chini ya hukumu.... ya dhamiri !

No comments:

Post a Comment