Thursday 10 July 2014

Tuamrishane mema

Mtoto alimuomba mamake amueleze kwa ufupi ujuzi wake na hikma alopata maishani, mamake akwambia: "utaweza kusikiliza?"

Akajibu: ndio......

Mama akasema:

Mwanangu: jichunge na kuzungumzia watu au mambo hadi uhakikishe ukweli wake, na akikujia mtu na habari yoyote hakikisha kabla kukimbilia......!

Na jihadhari na uvumi
Usiamini kila linalosemwa, wala nusu ya unayoyaona, na Allah akikuonja kwa adui pambana naye kwa kumfanyia hisani... sukuma uovu wake kwa lililo jema, nakuapia kwa Allah uadui utageuka mapenzi...

Ukitaka kumjua undani rafiki; safiri naye!
Safarini mtu hudhihirika uhakika wa undani wake....

Watu wakikuhujuma nawe uko kwenye haki furahia; kwasababu ni kama wanasema wewe umefaulu na unaathiri, kwani mbwa akiyekufa hapigwi teke, na haupurwi ila mti unaozaa matunda....!!

Mwanangu: ukitaka kuchagua mtu... mtazame kwa jicho la nyuki na usitazame watu kwa jicho la nzi kuangalia ubaya tu ulipo!

Lala mapema mwanangu kwani baraka ya rizki ni asubuhi, nakuhofia uikose riziki ya Allah Alrahman kwa kuwa unakesha....

Na nitakuhadithia kisa cha mbuzi na mbwa mwitu ili usimuamini anayefanya hila. Na mtu akikuamini, basi chunga tena chunga usimkhuni.....!

Nitakupeleka kwenye nyumba ya simba nikuoneshe kuwa simba hakuwa mfalme wa msitu kwa kuwa ananguruma ! Lakini ni kwasababu yeye ana ezi ya nafsi, hali windo la mwenzake hata akawa na njaa sana, basi usiibe juhudi ya mwenzako ukawa dhalimu....!!

Nitakupeleka kwa kinyonga, ili uone mwenyewe hila zake.! Anajigeuza rangi kwa rangi ya sehemu aliyo, ujue katika watu pia kuna mfano wake.....!!

Jizoeshe kushukuru mwanangu.......
Mshukuru Mwenyezi Mungu inatosha kuwa wewe ni Muislamu, inatosha kuwa unatembea, unasikia, unaona,,,,,,,,,,, mshukuru Mwenyezi Mungu na uwashukuru watu.. Mwenyezi Mungu anawazidishia wenye shukrani.. na watu wanapenda wakimpa mtu ashukuru.

Sifa njema kubwa katika maisha ni UKWELI.... na jua kwamba uongo hata ukiokoa ni muovu kabisa katika sifa mbovu...

Mwanangu.... jiwekee badala ya kila kitu, jitayarishe kwa jambo lolote, ili usidhalilike na kudharaulika.

Na ufaidike na fursa yoyote unayoipata sasa, huenda usiipate tena.

Usilalamike wala usijidhalilishe !! Nataka uwe mwenye hisia chanya uyakabili maisha, wakimbie wanaokata tamaa na wenye hisia hasi... na jihadhari kukaa na mtu anayepiga bao...!!

Usifurahie msiba wa mwenzako, na jihadhari na kumdharau mtu kwa umbo lake, kwani hakuna aliyejiumba.! Na katika kufanya dharau unakuwa unamfanyie aliye umba.

Kwa mafunzo na faida.... matatu:

-Usichukue vitu vitatu mpaka uviulizie:
Asali, dini, na mke.

-na vitatu hutapumzika hadi vikuepuke:
Wasiwasi, deni, na rafiki muovu.

- na vitatu vikichelewa vinakuwa havina faida:
Walima, taaziya na sala ya maghrib.

- na watatu Mungu akulinde nao:
Mwana wa haramu, mkata kizazi, na mla riziki ya mayatima.

-na watatu jiepushe na kuandamana nao:
Aso na akili, aso jali, aso na utu.

-na watatu usiwasikize:
Muongo, mfitinishaji, na mtoa ushuhuda wa uongo.

-na watatu usiwafanye marafiki:
Hasidi, na mwenye kijicho, na mwenye kukasirisha wazazi.

-na watatu usivunje rai zao:
Mwenye kuhifadhi sala yake, na mkarimu, na mwenye kuridhisha wazazi.

TUAMRISHANE MEMA

No comments:

Post a Comment