Thursday 10 July 2014

Tupunguzeni israfu na tuwasaidie maskini

Ni mara ngapi unafanya israfu ya chakula?

Ni mara ngapi unakitupa chakula kilichobaki kwa kuwa hamkitaki wala hakijaharibika?

Ni mara ngapi ni mwenye kuwalisha wenye nacho na kuwasahau maskini na mafukara wenye kulala na njaa?

Watoto wangapi wanakufaa kwa sababu ya njaa?

Tuko wapi Ummat Muhammad? Kwa nini usijipangie kawaida ya kutoa kwa kuwa unacho au kila pale utakapopata?

Nyoyo zimejaa tamaa hatutosheki na tunavyoruzukiwa. Muislamu anatupa nguo hali ya kuwa jirani yake hana cha kuvaa au muislamu mwenzake nchi za kimaskini hana cha kukivaa?

Tukumbuke hizo ni neema kwa Allah na tutakuja kuulizwa. Au tunasubiri watokezee wakristo ndio waje kuwasaidia waislamu ?

Sayyidina Othmaan alitoa sadaka ya msafar mzima wa biashara yake kwa waislamu wenye njaa. Hivi muislamu anaweza kusema hatonunua nguo kwa sababu anazo nyingi bali atoe sadaka?

au atatamani na yeye anunue ili azidi kujifakhirisha?

Ukifa unaenda na sanda tu huendi na viatu vyako wala nguo zako tanguliza mema kwa ajili ya maisha ya akhera. Mwanamke anaweka kanga zinafika pea 100 au mwanamme anaweka kanzu au nguo nyengine tele wallah kuna watu wanahitaji mvao mmoja au nguo moja tu ili ajistiri na mjuislamu anayajua ila moyo wake haushtuki. Raha yake ajaze nguo kabatini.

Subhana Allah wapi tunakwenda enyi waislamu?

Kwa nini tusikae tukawaza mambo ya kheri?

Tufanyeni haya kwa ajili ya Allah na si kujionesha.

Tukumbukeni aya za Allah zifuatazo :

"Tena bila ya shaka mtaulizwa siku hiyo juu ya neema." (8:102)

"Ogopeni Siku Ambayo Mutarudishwa Kwa Allah Kisha Kila Nafsi Italipa Kila Lile Ililochuma Na Wao Hawatadhulumiwa"(2:281)

Mtume Muhammad s.a.w anatwambia katika hadith refu ilopokelewa na Imamu Muslim, kua mja ataambiwa na Allah "Ewe mja wangu nilikutaka unilishe lakini hukunilisha, Mja atasema vipi nitakulisha hali ya kua wewe ndie Mola wa viumbe vyote?

Allah atamuambia;Jee hukujua kua mja fulani alihitaji umlishe lakini hukumlisha? Jee hujajua kama ungelimlisha basi ungelilikuta hilo kwangu?"

Nitakutumieni video yenye kutoa chozi juu ya misiba iliyowahi kuwakuta somalia. Halafu tuseme na nafsi zetu juu ya hali hizo.

No comments:

Post a Comment