Thursday 10 July 2014

Zingatia haya yatakusaidia katika maisha yako..

Kitu kizuri na chenye manufaa duniani ni kuilea nafsi iwe yenye kuridhika na kushukuru, na kuwa na nia safi.

Na hakuna kitu chema chenye kuleta faida kama kuwasamehe WENZAKO wote wenye kukukosea na wenye kukuchukia!

Lakin kuna jambo jingine bora zaidi hata Mtume
(S.A.W.) aliwahi kumuusia mmoja kati ya swahaba wake zaidi ya mara 3,
na kila mara alirudia akisistiza:

"USIKASIRIKE!"
"USIKASIRIKE!"
"USIKASIRIKE!"

Kwani hasira huzaa Chuki,
Chuki huzaa maudhi,
Maudhi huzaa kisirani, na
Kisirani huondosha nuru njema maishani na
huondosha mapenzi, maelewano, utulivu, na amani.

Tuazimie kutenda mema na Mungu Atatujaalia tawfiq,

In Sha Allah

1 comment: