Wednesday 24 June 2015

Fadhila za kumsalia Mtume saw

Imeandikwa na alhidaaya.com

Allaah سبحانه وتعالى Anasema,

((إِنَّ اللَّهَ وَمَلَائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى النَّبِيِّ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا صَلُّوا عَلَيْهِ وَسَلِّمُوا تَسْلِيمًا))

((Hakika Allaah Anamteremshia Rehma Mtume; na Malaika Wake (wanamuombea du'aa kwa vitendo vizuri alivyovifanya), Enyi mlioamini! Mswalieni (Mtume - muombeeni Rehma) na muombeeni amani)) [ Al-Ahzaab:56]

 

 

Hii ni amri kutoka kwa Allaah سبحانه وتعالى tumswalie Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na juu ya hivyo kuna fadhila kubwa kumswalia kwake kamailivyothibiti katika Hadiythi nyingi zifuatazo:

 عنْ عبد اللَّه بن عمرو بن العاص ، رضي اللَّه عنْهُمَا أنَّهُ سمِع رسُول اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم يقُولُ : ((من صلَّى عليَّ صلاَةً ، صلَّى اللَّه علَيّهِ بِهَا عشْراً))   رواهُ مسلم

Imetoka kwa 'Abdullaah bin 'Amru bin Al'-Aasw رضي اللَّه عنْهُمَا kwamba kamsikia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم anasema, ((Atakayeniswalia (atakayeniombea) mara moja Allaah Atamswalia (Atampa rahma) mara kumi)) [Muslim]

Subhaana Allaah! Hii ni fadhila tukufu kabisa kwamba Mola Aliyetuumba Atuswalie sisi waja wake mara kumi tutakapomswalia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم mara moja tu! Ukipima utaona fadhila hii haimkalifu mtu zaidi ya dakika moja!

 

Maana ya Swalah ya Allaah سبحانه وتعالى na Malaika Wake

Swalah ya Allaah سبحانه وتعالى  kwa waja Wake ni: Rahma na kuwasifu kwa Malaika.

Swalah ya Malaika kwa Waumini  ni: du'aa na kuwaombea Maghfirah.

عن ابن مسْعُودٍ رضي اللَّه عنْهُ أنَّ رسُول اللَّهِ صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم قال : (( أَوْلى النَّاسِ بي يوْمَ الْقِيامةِ أَكْثَرُهُم عَليَّ صلاةً)) رواه الترمذي وقال : حديثٌ حسنٌ

Imetoka kwa ibn Mas'uud رضي اللَّه عنْهُkwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلمamesema,

((Watu wa mwanzo kwangu (watakaokuwa karibu yangu) siku ya Qiyaamah ni wale wanaoniswaliasana))  [At-Tirmidhy na kasema ni Hadiythi Hasan]

 

Fadhila nyingine hii ya kuwa karibu kabisa na Mtume  wetu mpenzi  صلى الله عليه وآله وسلم. Nani asiyetaka kuwa na karibu naye siku ya Qiyaamah?

 عن أوس بن أوس ، رضي اللَّه عنْهُ قال : قالَ رسولُ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم : (( إنَّ مِن أَفْضلِ أيَّامِكُمْ يَوْمَ الجُمُعةِ ، فَأَكْثِرُوا عليَّ مِنَ الصلاةِ فيه ، فإنَّ صَلاتَكُمْ معْرُوضَةٌ علَيَّ)) فقالوا : يا رسول اللَّه ، وكَيْفَ تُعرضُ صلاتُنَا عليْكَ وقدْ أرَمْتَ ؟ ، يقولُ : بَلِيتَ ، قالَ: (( إنَّ اللَّه حَرم على الأرْضِ أجْساد الأنْبِياءِ )) . رواهُ أبو داود بإسنادٍ صحيحِ

Imetoka kwa Aws ibn Aws   رضي اللَّه عنْهُ kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema ((Siku iliyo bora kabisa kwenu ni siku ya Ijumaa, kwa hiyo zidisheni kuniswalia (siku hiyo) kwani Swalah zenu zinaonyeshwa kwangu)) Wakasema (Maswahaba) Ewe Mjume wa Allaah vipi Swalah zetu zinaonyeshwa kwako na hali utakuwa umeoza?  Akasema, ((Allaah Ameharamisha ardhi kuila miili ya Mitume)) [Abu Daawuud kwa isnaad ya Sahiyh]

 عنْ أبي هُريْرةَ رضي اللَّه عنهُ قال : قال رسُولُ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم : (( رَغِم أنْفُ رجُلٍ ذُكِرْتُ عِنْدَهُ فَلَمْ يُصَلِّ علَيَّ))  رواهُ الترمذي وقالَ : حديثٌ حسنٌ .

 

Imetoka kwa Abu Hurayrah رضي اللَّهkwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلمamesema, ((Amepata khasara mtu ambaye nimetajwa kwake na hakuniswalia)) [At-Tirmidhiy na kasema Hadiyth Hasan]

 عنْ أبي هُريْرةَ رضي اللَّه عنهُ أنَّ رسُولَ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم قال : (( ما مِنْ أحد يُسلِّمُ علَيَّ إلاَّ ردَّ اللَّه علَيَّ رُوحي حَتَّى أرُدَّ عَليهِ السَّلامَ )) . رواهُ أبو داود بإسناد صحيحٍ

Imetoka kwa Abu Hurayrah رضي اللَّهkwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلمamesema,

((Yeyote atakayeniswalia hurudishiwa roho yangu hadi nimrudishie salaam))[Abu Daawuud kwa isnaad ya Hasan]

 

Ni jambo la ajabu kwetu kuwa roho yake Mtume صلى الله عليه وآله وسلمhurudishiwa kwa ajili ya kujibu salaam zetu tu.

 وعن علِيٍّ رضي اللَّه عنْهُ قال : قال رسُولُ اللَّهِ صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم : (( الْبخِيلُ من ذُكِرْتُ عِنْدَهُ ، فَلَم يُصَلِّ علَيَّ )) رواهُ الترمذي وقالَ : حديثٌ حسنٌ صحيحٌ .

Imetoka kwa 'Aliy رضي اللَّه kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلمamesema, ((Bakhili ni yule ambaye nimetajwa kwake na hakuniswalia))[At-Tirmidhiy na kasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

Bila shaka hakuna anayependa kuwa na sifa hiyo, na sio ubakhili wenye uhusiano na  fedha bali ni kwa kutokumswalia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم.

 

Vipi kumswalia Mtume?صلى الله عليه وآله وسلم

 عنْ أبي مسْعُود الْبدْريِّ ، رضي اللَّه عنْهُ ، قالَ : أَتاناَ رسُولُ اللَّهِ صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم ، وَنَحْنُ في مَجْلِس سعد بنِ عُبَادَةَ رضي اللَّه عنهُ ، فقالَ لهُ بَشِيرُ بْنُ سعدٍ : أمرَنَا اللَّه أنْ نُصلِّي علَيْكَ يا رسولَ اللَّهِ ، فَكَيْفَ نُصَّلي علَيْكَ ؟ فَسكَتَ رسولُ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم ، حتى تَمنَّيْنَا أنَّه لمْ يَسْأَلْهُ ، ثمَّ قال رسولُ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم  (( قولُوا : اللَّهمَّ صلِّ عَلى مُحَمَّدٍ ، وَعَلى آلِ مُحمَّدٍ ، كما صليْتَ على آل إبْراهِيم ، وَبارِكْ عَلى مُحَمَّد ، وعَلى آلِ مُحمَّد ، كما بَاركْتَ عَلى آل إبْراهِيم ، إنكَ حمِيدٌ مجِيدٌ ، والسلام كما قد عَلِمتم ))رواهُ مسلمٌ

Imetoka kwa Abu Mas'uud Al-Badriyرضي اللَّه عنْهُ ambaye amesema, alitujia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na sisi tulikuwa katika majlis (ukumbi) wa Sa'ad ibn 'Ubaadah رضي اللَّه عنْهُ Bashiyr ibn Sa'ad akamwambia, Allaah Ametuamrisha tukuswalie ewe Mjumbe wa Allaah, je, Vipi tukuswalie? Akanyamaza Mtume صلى الله عليه وآله وسلم mpaka tukatamani kwamba asingelimuuliza. Kisha akasema Mtume صلى الله عليه وآله وسلم((semeni: Allaahumma Swalli 'Alaa Muhammadin Wa 'alaa aali Muhammadin Kamaa Swallayta 'alaa aali Ibraahiym, Wa Baarik 'alaa Muhammadin Wa 'alaa aali Muhammadin Kama Baarakta 'alaa aali Ibraahiym Innaka Hamiydum-Majiyd. Na salaam kamamlivyofundishwa)) [Muslim]

 

Basi ndugu Waislamu tusiziache fadhila tukufu na nyingi kama hizo kwa kumswalia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kila mara, ndimi zetu ziwe daima zikimswalia na kufanya hivyo pia  inaingia katika fadhila za kumkumbuka Allaah سبحانه وتعالى. 

 

Allaahumma Turuzuku mapenzi Yako na mapenzi ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na Tujaaliye tuwe karibu yake katika Pepo ya Firdaws.  Allaahumma  Mpe Mtume Muhammad صلى الله عليه وسلم)  wasila, na fadhila, na Mfikishe daraja yenye kusifiwa, ambayo Umemuahidi.

 

No comments:

Post a Comment